JAMII YASHAURIWA KUWASAIDIA WATOTO YATIMA.


TAREHE 03-01-2018.


Jamii  nchi imeshauriwa kuanza mwaka wa 2018 kwa kuwasaidia watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu kwa kuw ajukumu la kuwalea watoto hao ni la kila mmoja.

Ushauri huo umetolewa na msemaji wa kikundi cha Friends of Batuli Bi Batuli Isaya wakati akitoa misaada mbali mbali  ya chakula ,mavazi pamoja na msaada wa kuvuta majitaka  katika kituo cha kulelea watoto yatima cha Good Hope Kiwawa Children kilichopo wilayani Arumeru kwa lengo la kuwatia moyo na kuwatatulia changamoto zinazowakabili kituoni hapo katika mwaka huu mpya wa 2018.

Bi Batuli Amesema kuwa ni vyema jamii ikajiwekea utaratibu wa kushirikiana  na wanaharakati wengine katika kutatua changamoto za watoto yatima kwa kikundi au kwa mtu mmoja mmoja na  kuchangishana kidogo kidogo na hatimae wakaweza kutatua changamoto zinazowakabili watoto yatima.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa kituo hicho Ombeni Palangyo amesema kuwa kituo hicho kimekuwa kikiwalea watoto yatima na kuwapeleka shule lakini bado kina changamoto zinazokabiliwa nazo ikiwemo vifaa vya shule na hivyo kuitaka jamii kuungana kwa pamoja kujitolea katika kusaidia watoto hao wenye uhitaji kama walivyofanya kikundi hicho cha friends of Batuli.
JAMII YASHAURIWA KUWASAIDIA WATOTO YATIMA. JAMII YASHAURIWA KUWASAIDIA WATOTO YATIMA. Reviewed by safina radio on January 03, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.