WATU 7 WAFARIKI NCHINI ETHIOPIA

TAREHE 22-01-2018
Polisi Ethiopia wakikabiliana na raia
Image caption
Watu saba wamekufa huko Ethiopia kaskazini baada ya vikosi vya usalama kufyatua risasi kwenye mkusanyiko wa watu waliohudhuria tamasha la kidini siku ya jumamosi.
Vifo hivyo katika mji wa Waldiya vimesababisha maandamano ya siku mbili yaliyosababisha uharibu wa nyumba, magari na barabara kufungwa .
Mashuhuda wanasema ghasia hizo zilianza  siku ya jumamosi pale waumini hao walipoanza kuimba nyimbo za kuipinga serikali na ndipo vikosi vya serikali vilianza kuwafyatulia risasi na kusababisha majeraha na vifo.

Waandamanaji wenye hasira walianza kuchoma magari,nyumba na biashara za wale wanaodhaniwa kuunga mkono serikali,ambapo waandamanaji kadhaa wanashikiliwa na Polisi.


WATU 7 WAFARIKI NCHINI ETHIOPIA WATU 7 WAFARIKI NCHINI ETHIOPIA Reviewed by safina radio on January 22, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.