BODI YA MIKOPO YA ELIMU YA JUU YAKUSANYA BILIONI 85 .
TAREHE 03-01-2018
Bodi
ya mikopo ya elimu ya juu hapa nhcini imesema kuwa imekusanya kiasi cha shilingi
bilioni 85 hadi kufikia Disemba mwaka jana kutoka kwa wanufaika wa mikopo ikiwa
ni sawa na asilimia 66 ya lengo la kukusanya shilingi bilioni mia moja na
thelathini kwa mwaka wa fedha wa 2017-2018.
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini dar-es-salaam mkurugenzi mtendaji wa bodi hiyo Bw
Abdurazaki Badru amesema kuwa katika zoezi la kuwasaka wadaiwa wa mikopo
wamebainika wanufaika wengine elfu ishirini na sita na kufanya wanufaika wa
mikopo hapa nchini kufikia laki moja na elfu ishirini na moja.
Amesema
kuwa ili kufikia lengo walilojiwekea kwa mwaka wameweka mikakati mbalimbali ya
kuongeza ukusanyaji wa mapato kutoka shilingi bilioni 13 kwa mwezi hadi
shilingi bilioni 17 kwa mwezi.
Katika
hatua nyingine mkurugenzi huyo amesema kuwa katika kipindi cha miezi sita
wamekamilisha shughuli za utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza takribani elfu thelathini na tatu mia nne na
ishirini na nne yenye thamani ya shilingi bilioni mia moja na kumi.
Hata
Bw Badru ameongeza kuwa wanafunzi wanaotakiwa kupatiwa mikopo ni laki moja na ishirini
na mbili wa mwaka wa kwanza hadi mwaka wa tatu kwa bajeti ya shilingi biloni
mia nne na ishirini na mbili.
BODI YA MIKOPO YA ELIMU YA JUU YAKUSANYA BILIONI 85 .
Reviewed by safina radio
on
January 03, 2018
Rating:
No comments