MAREKANI YATISHIA KUKATA MSAADA WA KIFEDHA KWA SERIKALI YA PALESTINA.

TAREHE 03-01-2018
Rais wa Marekani Donald Trump ametishia kukata msaada wa kifedha kwa serikali ya Palestina, kwa maelezo kwamba Marekani inawalipa mamia ya mamilioni ya dola za kimarekani kwa mwaka na hakuna chochote inachoambulia na hakuna  heshima kutoka kwa taifa hilo.
Katika utamaduni aliojijengea rais wa Marekani wa matumizi wa mtandao wa kijamii wa twitter kama sehemu yake ya kutolea matamko , rais huyo amesema kwamba Wapalestina hawana mpango wowote wa kuwa na mazungumzo ya maridhiano na amani na Israel na kuhoji uhalali wa Marekani kuendelea kujitoa kwa kiasi hicho.

Mwezi uliopita rais wa Palestina Mahmoud Abbas alitoa tamko la taifa lake kutokuwa tayari kupokea mpango wowote wa amani kutoka Marekani, baada ya mji wa Washington kuitambua Yerusalemu kama mji mkuu wa Israeli.
MAREKANI YATISHIA KUKATA MSAADA WA KIFEDHA KWA SERIKALI YA PALESTINA. MAREKANI YATISHIA KUKATA MSAADA WA KIFEDHA KWA SERIKALI YA PALESTINA. Reviewed by safina radio on January 03, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.