WAZIRI NDALICHAKO AMSIMAMISHA KAZI MKUU WA KITENGO CHA UNUNUZI CHUO KIKUU MUHIMBILI.
TAREHE 18-01-2018
Waziri wa elimu sayansi tekinolojia na
mafunzo ya ufundi Professa Joyce Ndalichako amemsimamisha kazi mkuu wa kitengo
cha ununuzi wa chuo kikuu cha afya na sayansi ya tiba Muhimbili (MUHAS) Bw Nuru
Mkali ili kupisha uchunguzi kutokana na tuhuma za kukiuka utaratibu wa ununuzi.
Professa Ndalichako ametangaza uamuzi
huo jijini Dar-es-salaam katika mkutano wake na watendaji wa chuo kikuu cha
afya na sayansi ya tiba Muhimbili mara baada ya kutembelea chuo hicho,ambapo
pia ameiagiza bodi ya MUHAS kuwa makini na watendaji wasiokuwa waaminifu.
Amesema kuwa hakuna kitu kinaumiza na
kuudhi kama mtu anayefanya madudu akidhani kama serikali iko usingizini hivyo
ameamua mkuu wa kitengo cha manunuzi kusimamishwa kazi mara moja pamoja na watu
wengine wanaohusika kufanya manunuzi bila utaratibu.
Kwa upande wake mwenyekiti wa bodi ya
chuo hicho Bi Mariamu Mwafisi amesema kuwa mara baada ya uchunguzi kukamilika
kuhusu sakata hilo watendaji wote waliohusika watachukuliwa hatua za kisheria.
Hata hivyo mtendaji aliyesimamishwa
kazi anatuhumiwa kununua vifaa vya chuo kwa kupitia kampuni tatu ambazo
zinamilikiwa na mtu mmoja huku baadhi ya vifaa vikinunuliwa bila kuhitajika.
WAZIRI NDALICHAKO AMSIMAMISHA KAZI MKUU WA KITENGO CHA UNUNUZI CHUO KIKUU MUHIMBILI.
Reviewed by safina radio
on
January 19, 2018
Rating:

No comments