MAHAKAMA NCHINI BRAZIL YAREFUSHA HUKUMU YA RAIS WA ZAMANI WA NCHI HIYO LUIZ INACIO LULA DASILVA
TAREHE 25-01-2018
Mahakama ya rufaa
nchini Brazil imeshikilia hukumu ya makosa ya rushwa iliyotolewa dhidi ya rais
wa zamani wa nchi hiyo Luiz Inacio Lula da Silva, hatua ambayo ni pigo kubwa
kwa matumaini yake ya kugombea tena katika uchaguzi wa mwaka huu.
Jopo hilo la majaji
watatu limefanya uamuzi wa kauli moja kuwa hukumu yake ya awali ya miaka tisa
na nusu jela irefushwe hadi zaidi ya miaka 12.
Lula ambaye ana umri
wa miaka 72, ameuambia umati wa karibu watu elfu kumi kuwa ananuia kugombea uchaguzi wa
rais licha ya kikwazo hicho cha mahakama.
Hata hivyo Anatarajiwa
kuendelea kupinga hukumu hiyo kupitia mahakama za juu, kwanza katika Mahakama
Kuu ya Haki na kisha Mahakama ya Juu kabisa ya Brazil.
MAHAKAMA NCHINI BRAZIL YAREFUSHA HUKUMU YA RAIS WA ZAMANI WA NCHI HIYO LUIZ INACIO LULA DASILVA
Reviewed by safina radio
on
January 25, 2018
Rating:

No comments