BALOZ SEIF ALLY IDD AMESEMA ZANZIBAR INATAMBUA MCHANGO UNAOTOLEWA NA ASASI ZA KIRAIA
TAREHE 25-01-2018
Makamu wa pili wa rais wa serikali ya mapinduzi ya
Zanzibar Balozi Seif Ally Idd amesema kuwa Zanzibar inatambua na kuthamini
mchango unaotolewa na asasi za kiraia katika maendeleo ya taifa na ipo tayari
kufanya kazi na asasi hizo.
Balozi Seif amesema hayo mjini Zanzibar katika
kongamano lililokutanisha asasi mbalimbali za kiraia visiwani humo lengo likiwa
ni kujadiliana na kubadilishana uzoefu na kuona namna ya kuziendeleza asasi
hizo.
Amesema kuwa ni wazi kwamba pale penye ushirikiano
mzuri baina ya serikali na asasi kiraia maendeleo kwa urahisi zaidi na siku
zote serikali na asasi hizo zinajenga nyumba moja na mafaniko yao ndio
mafanikio ya wananchi.
Kwa upande wake mkurugenzi wa TAMWA kutoka Zanzibar
Bi Mzuri Issa amesema kuwa asasi za kiraia ziko tayari kufanya kazi na serikali
kinachotakiwa ni ushirikiano na kupitia kongamano hili wamejadili mambo
mbalimbali ikiwemo namna ya kuziendeleza asasi hizo kwa kubadilishana uzoefu.
BALOZ SEIF ALLY IDD AMESEMA ZANZIBAR INATAMBUA MCHANGO UNAOTOLEWA NA ASASI ZA KIRAIA
Reviewed by safina radio
on
January 25, 2018
Rating:

No comments