WIZARA YA MAMBO YA NJE YA MAREKANI YATANGAZA KUZUIA DOLA MILIONI 65 .

TAREHE 17-01-2018

Wizara ya mambo ya nje ya Marekani imetangaza kuwa itazuia kiasi cha dola milioni 65 kati ya dola milioni 125 ilizopanga kutoa kama mchango wake kwa ajili ya ufadhili katika shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na misaada wakati wa masuala ya dharura.

Wizara hiyo ya mambo ya nje ya Marekani imesema misaada yoyote itakayotolewa katika siku zijazo sasa itategemea iwapo shirika hilo litafanya mabadiliko makubwa katika utendaji wake.

Licha ya tangazo hilo Marekani bado inatarajia kuidhinisha kiasi cha dola milioni 60 ili kuzuia shirika hilo lisipungukiwe na fedha kabla ya kufikia mwishoni mwa mwezi huu.

Marekani imesema bado inasubiri uamuzi kuhusiana na kile ilichoeleza sera zinazoeleweka kuhusiana na Palestina kabla ya kuidhinisha malipo zaidi.

Marekani ndio mfadhili mkuu wa shirika hilo ikitoa karibu asilimia 30 ya bajeti ya kila mwaka ya shirika hilo ambalo pia uhudumia kiasi ya wapalestina milioni 5 waliolazimika kuyahama makazi yao kutokana na mzozo wa muda mrefu kati ya Palestina na Israel.




WIZARA YA MAMBO YA NJE YA MAREKANI YATANGAZA KUZUIA DOLA MILIONI 65 . WIZARA YA MAMBO YA NJE YA MAREKANI YATANGAZA KUZUIA DOLA MILIONI 65 . Reviewed by safina radio on January 17, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.