NAIBU WAZIRI WA UJENZI ELIAS KWANDIKWA AMEITAKA TANROADS KUHAKIKISHA WANAWEKA MIZANI YA KUHAMISHIKA KATIKA ENEO LA MAKAMBAKO
TAREHE 19-01-2018
Naibu waziri wa ujenzi Mh Elias
Kwandikwa amewaagiza Wakala wa barabara hapa nchini TANRODS kuhakikisha kuwa
ndani ya mwezi mmoja wanaweka mizani ya kuhamishika katika eneo la mizani la
Makambako ili kutatua changamoto ya msongamano wa magari katika eneo hilo.
Mh Kwandikwa ametoa maagizo hayo mkoani Njombe mara baada ya kutembelea mizani
hiyo na kujionea changamoto ya foleni ya magari katika eneo hilo.
Aidha naibu waziri huyo amewaonya
madereva wote wanaotumia kisingizio cha uwepo wa foleni katika mizani hiyo na
kufanya mambo yao binafsi.
Hata hivyo Mh Kwandikwa amemaliza
ziara yake ya kikazi katika mikoa ya Lindi,Ruvuma,Mtwara na Njombe ambapo
ameweza kutembelea na kukagua miradi mbalimbali inayotekelezwa na wizara yake.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI ELIAS KWANDIKWA AMEITAKA TANROADS KUHAKIKISHA WANAWEKA MIZANI YA KUHAMISHIKA KATIKA ENEO LA MAKAMBAKO
Reviewed by safina radio
on
January 19, 2018
Rating:

No comments