CHAMA CHA ANC KUFANYA UCHAGUZI KUMTAFUTA MRITHI WA RAIS JACOB ZUMA.

TAREHE 18-12-2017


Chama tawala cha Afrika Kusini, African National Congress, ANC kinapiga kura ya kumchagua mrithi wa Rais Jacob Zuma.

Wachambuzi wanasema kinyang'anyiro cha uongozi wa chama cha ANC ni kikali mno kati ya Makamu wa Rais Cyril Ramaphosa na mke wa zamani wa Zuma na ambaye ni waziri wa zamani Nkosazana Dlamini-Zuma.

 Bontle Mpakanyane kutoka tume ya uchaguzi ametangaza kuwa viongozi hao wawili ndio wagombea pekee katika kinyang'anyiro cha mwisho.
ANC ilichelewesha uchaguzi huo kutokana na mgogoro kuhusiana na wajumbe wanaoruhusiwa kushiriki katika zoezi hilo.

Hata hivyo  Uchaguzi huo unafanyika wakati kukiwa na kashfa na tuhuma za rushwa ambazo zimechafua mihula miwili ya urais wa Zuma na chama cha ANC baada ya kuwa madarakani kwa miaka 23.


CHAMA CHA ANC KUFANYA UCHAGUZI KUMTAFUTA MRITHI WA RAIS JACOB ZUMA. CHAMA CHA ANC KUFANYA UCHAGUZI KUMTAFUTA MRITHI WA RAIS JACOB ZUMA. Reviewed by safina radio on December 18, 2017 Rating: 5

No comments