MKUTANO MKUU WA UMOJA WA MATAIFA WAPINGANA NA RAIS TRUMP
TAREHE 22-12-2017
Mkutano mkuu wa Umoja wa mataifa umepiga Kura ya kutoyatambua maamuzi ya Marekani ya kuutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel.
Mkutano mkuu wa Umoja wa mataifa umepiga Kura ya kutoyatambua maamuzi ya Marekani ya kuutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel.
Makubaliano hayo ya mkutano wa umoja wa
mataifa yamefikiwa pamoja na vitisho vya Rais wa Marekani Donald Trump
aliyetishia kuzikatia msaada wa kifedha nchi zote zitakazopinga msimamo wake.
Mataifa mia moja ishirini wameyapigia
kura maazimio, yakiwamo mataifa ambayo
ni washirika wa karibu wa marekani kama Japan, Uingereza na Ujerumani.
Canada na Mexico ni moja ya mataifa
thelathini na tano ambayo hayakuhudhuria mkutano huo,ambao Wapalestina wamesema
hatua hiyo ya Umoja wa mataifa kuwa ni ushindi wa
Palestina ingawa Israel imeyakataa matokeo hayo .
Kabla ya kura hiyo balozi wa marekani katika umoja wa mataifa, Bi
Nikki Haley alionya kuwa Marekani haitasahau au kusamehe pale nchi zilizoipinga
Marekani zitakapoenda kuomba misaada.
MKUTANO MKUU WA UMOJA WA MATAIFA WAPINGANA NA RAIS TRUMP
Reviewed by safina radio
on
December 22, 2017
Rating:
No comments