WAZIRI WA NISHATI MERNAD KALEMANI AMESEMA KUWA VIJIJI VYOTE KATIKA JIMBO LA MTERA KUPATA UMEME.

TAREHE 22-12-2017


Waziri wa nishati hapa nchini Mh Mernad Kalemani amesema kuwa mradi wa uwekaji umeme vijijini awamu ya tatu itaweka umeme katika vijiji na kata zote za jimbo la Mtera mkoani Dodoma.

Mh Kalemani ameyasema hayo wakati wa ziara yake ya kujionea kazi ya usambazaji umeme vijijini REA awamu ya tatu inavyoendelea katika jimbo hilo pamoja na kusikiliza kero za wananchi.

Amesema mbali na mradi huo kuweka umeme kwenye taasisi,mashirika,pamoja na masoko utawekwa pia kwenye nyumba za wakazi wote ambao wameshalipia gharama za kuunganishiwa huduma hiyo bila kusahau makanisa na misikiti.


Kwa upande wake mbunge wa Mtera Mh Livingstone Lusinde amesema kuw akutokuwepo kwa umeme katika jimbo hilo imerudisha nyuma jitihada za kuanzisha miradi mbalimbali za maendeleo.
WAZIRI WA NISHATI MERNAD KALEMANI AMESEMA KUWA VIJIJI VYOTE KATIKA JIMBO LA MTERA KUPATA UMEME. WAZIRI WA NISHATI MERNAD  KALEMANI  AMESEMA KUWA  VIJIJI VYOTE  KATIKA JIMBO LA MTERA KUPATA UMEME. Reviewed by safina radio on December 22, 2017 Rating: 5

No comments