NAIBU WAZIRI WA KILIMO NCHINI DK. MARY MWANJELWA ATOA SIKU SABA KWA MKURUGENZI WA BODI YA PARETO KUTOA MAJIBU YA KERO ZA WAKULIMA.
TAREHE 01 -12-2017
Naibu waziri wa Kilimo
Nchini Dk. Mary Mwanjelwa ametoa siku saba kwa Mkurugenzi wa Bodi ya Pareto
Nchini kuhakikisha wanatoa majibu ya
kero za wakulima wa zao hilo Wiliyani Mbeya ambao wamekosa imani na Bodi hiyo.
Dk. Mwanjelwa ametoa
muda huo kufuatia malalamiko ya wakulima wa zao la pareto kukosa mtetezi licha
ya serikali kuanzisha bodi hiyo kwa ajili ya kuwasaidia wakulima.
Aidha, Dk. Mwanjelwa
amemwagiza Mkurugenzi wa Bodi hiyo ya Pareto nchini kutoa majibu ndani ya siku
saba baada ya kufika Wilayani hapo.
Pia, Naibu Waziri huyo
wa Kilimo ameongeza kuwa inapaswa suala hilo lifike mwisho na kuhakikisha jinsi
ya kupanua wigo wa fursa za masoko kwa ajili ya kumbadilisha mkulima wa zao
hilo la pareto.
Hata hivyo, Tanzania ni
nchi ya pili Duniani na ya kwanza Barani Afrika kwa uzalishaji wa zao la pareto
na asilimia 80 ya zao hilo huzalishwa Wilayani Mbeya.
NAIBU WAZIRI WA KILIMO NCHINI DK. MARY MWANJELWA ATOA SIKU SABA KWA MKURUGENZI WA BODI YA PARETO KUTOA MAJIBU YA KERO ZA WAKULIMA.
Reviewed by safina radio
on
December 01, 2017
Rating:

No comments