WAZIRI WA UJENZI MAKAME MBARAWA AMEWATAKA WAKANDARASI WANAOJENGA RELI KUFANYA KAZI KWA UADILIFU.

TAREHE 13-12-2017
Image result for picha ya makame mbarawa mnyaa


Waziri  wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliano Profesa Makame Mbarawa  amewataka wakandarasi wanaojenga reli ya kisasa yaani standard gauge kufanya kazi kwa uadilifu ili kuwezesha mradi huo kukamilika kwa wakati.

Waziri Mbarawa ameyasema hayo mkoani Pwani wakati alipotembelea mradi huo katika kijiji cha Soga ambapo pia ameitaka kampuni hodhi ya rasilimali za reli RAHCO kufuatilia kwa karibu mradi huo ili ukamilike  ifikapo mwaka elfu mbili na ishirini.

Mh. Mbarawa amewataka wakandarasi hao kufanya kazi kwa uadilifu na viwango walivyokubaliana na serikali huku akiwataka wahandisi kuelewa kuwa wana wajibu mkubwa na chochote kikiharibika katika mradi huo wa ujenzi wa reli wa kwanza kulaumiwa ni wao.


Mradi wa reli ya kisasa unatekelezwa kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza unahusisha ujenzi wa reli kutoka Dar es salaam  hadi Morogoro, na ya pili kutoka Morogoro hadi Makutupora mkoani Dodoma na utakuwa na urefu wa kilomita mia saba ishirini na mbili na utagharimu kiasi cha shilingi trilioni 7.1.
WAZIRI WA UJENZI MAKAME MBARAWA AMEWATAKA WAKANDARASI WANAOJENGA RELI KUFANYA KAZI KWA UADILIFU. WAZIRI WA UJENZI MAKAME MBARAWA AMEWATAKA WAKANDARASI WANAOJENGA RELI KUFANYA KAZI KWA UADILIFU. Reviewed by safina radio on December 13, 2017 Rating: 5

No comments