VYAMA VINAVYOUNGA MKONO KUJITENGA KWA JIMBO LA CATALONIA VYASHINDA UCHAGUZI.

TAREHE 22-12-2017

VHaki miliki ya pichaREUTERS
Image caption

Vyama vinavyounga mkono jimbo la Catalonia kujitenga na Uhispania vimeshinda uchaguzi wa jimbo la Catalonia.
Ikiwa kura zote zinakaribia kukamillika kuhesabiwa Katika  uchaguzi ambao wapiga kura wengi wamejitokeza vyama hivyo vinaonekana kushinda japo vimepunguza kidogo idadi ya viti bungeni.
Matokeo hayo kwa vyovyote ni habari mbaya kwa waziri mkuu wa Hispania,Mariano Rajoy ambaye aliingilia kati jimbo hilo kujitenga hivi karibuni na kuitisha uchaguzi huo.

Akiwa uhamishoni mjini Brussels aliyekuwa rais wa Catalonia ,Carles Puigdemont amepongeza matokeo hayo na kusema ni ushindi wa demokrasia kwa sababu ya idadi kubwa ya watu walijitokeza kupiga kura na kusema hakuna wa kuyapinga.
Hata hivyo baada ya uchaguzi huo tatizo kubwa kwa pande zote ni kwamba hakuna uhakika kuwa uchaguzi huo na matokeo hayo yanaweza kutatua mgogori huo unaoendelea baina ya Catalonia na serikali ya Madrid.









VYAMA VINAVYOUNGA MKONO KUJITENGA KWA JIMBO LA CATALONIA VYASHINDA UCHAGUZI. VYAMA VINAVYOUNGA MKONO KUJITENGA KWA JIMBO LA  CATALONIA VYASHINDA UCHAGUZI. Reviewed by safina radio on December 22, 2017 Rating: 5

No comments