RAIS WA TANZANIA JOHN MAGUFULI AMEUTAKA UMOJA WA MATAIFA KUFANYA UCHUNGUZI KUBAINI CHANZO CHA VIFO VYA WANAJESHI 14.
TAREHE 14-12-2017

Amesema kuwa vifo vya walinda amani hao
vimesababisha majonzi makubwa kwa watanzania hivyo ni lazima umoja wa mataifa
ufanye uchunguzi wa kina na ulio wazi na haraka iwezekanavyo kuhusu vifo vya
wananjeshi hao ili ukweli uweze kujulikana na haki iweze kutendeka.
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia
ni amiri jeshi mkuu wa jeshi la ulinzi na usalama Mh John Magufuli ameutaka
umoja wa mataifa kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini chanzo kamili cha vifo vya
wananjeshi 14 wa Tanzania waliouawa wiki iliyopita wakati wakilinda amani huko
jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo.
Mh Magufuli ametoa kauli hiyo leo katika salamu zake
zilizotolewa kwa niaba yake na waziri mkuu Mh Majaliwa Kassim Majaliwa wakati
wa zoezi la kuaga miili ya wanajeshi hao liliofanyika katika viwanja vya jeshi jijini
Dar-es-salaam.

Kwa upande wakae waziri wa ulinzi na jeshi la
kujenga taaifa Mh Hussen Mwinyi amesema kuwa pamoja na vifo vya wananjeshi hao
jeshi la Tanzania halitakata tamaa katika kutimiza wajibu wao kama taifa huko
Kongo na maeneo mengine wanakotoa msaada wa kulinda amani.
Hata hivyo wanajeshi hao 14 wa Tanzania waliuawa wiki
iliyopita baada ya kutokea shambulizi la kushtukiza lililofanywa na waasi huko
nchini Kongo ambapo mbali na waliopoteza maisha wanajeshi wengine zaidi ya 40
walijeruhiwa katika tukio hilo.
RAIS WA TANZANIA JOHN MAGUFULI AMEUTAKA UMOJA WA MATAIFA KUFANYA UCHUNGUZI KUBAINI CHANZO CHA VIFO VYA WANAJESHI 14.
Reviewed by safina radio
on
December 14, 2017
Rating:

No comments