WAKURUGENZI WOTE HAPA NCHINI WAMETAKIWA KUTEKELEZA MIRADI YA UJENZI WA VITUO VYA AFYA, MADARASA NA NYUMBA ZA WAALIMU.

TAREHE 18-12-2017


Waziri wa nchi ofisi ya rais tawala za mikoa na serikali na za mitaa Mh Suleman Jaffo amewataka wakurugenzi wote hapa nchini kutekeleza miradi ya ujenzi wa vituo vya afya,madarasa,nyumba za waalimu na mabweni ya wanafunzi   kwa kutumia mfumo wa Force Account.

Mh Jaffo ametoa maagizo hayo baada ya kuridhishwa na utekelezwaji wa zahanati,madarasa pamoja na maabara unaotekelezwa kwa kutumia mfumo wa Force Account katika halmashauri ya wilaya ya Nzega mkoani Tabora ambao kwa ujumla utagharimu kiasi cha shilingi milioni mia sita hamsini na moja.

Amesema kuwa  wa mfumo wa Force Account ni mfumo unaowezesha serikali kutekeleza miradi yake ya maendeleo kwa kutumia mafundi walioko katika jamii badala ya wakandarasi wakubwa ambao hutumia gharama kubwa kujenga na kutekeleza miradi hiyo.

Ameongeza kuwa kutokana na kazi nzuri iliyofanywa na wilaya ya Nzega kuanzia sasa wakurugenzi wa halmashauri zote hapa nchini wanapaswa kutumia mfumo huo ili kuondoa matumizi mabaya ya fedha za serikali na pia kuwapa ajira mafundi wa ujenzi walioko katika jamii ya kitanzania.


Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Nzega Bw Godfrey Mkopula ameahidi kusimamia ipasavyo fedha za miradi mbalimbali inayotengwa na  serikali kwa maslahi ya wananchi wa wilaya hiyo.
WAKURUGENZI WOTE HAPA NCHINI WAMETAKIWA KUTEKELEZA MIRADI YA UJENZI WA VITUO VYA AFYA, MADARASA NA NYUMBA ZA WAALIMU. WAKURUGENZI   WOTE HAPA NCHINI WAMETAKIWA KUTEKELEZA MIRADI YA UJENZI  WA VITUO VYA AFYA, MADARASA NA NYUMBA  ZA WAALIMU. Reviewed by safina radio on December 18, 2017 Rating: 5

No comments