RAIS WA TANZANIA MH. JOHN MAGUFULI AMEITAKA BENKI KUU KUZIFUTA BENKI ZILIZOSHINDWA KUJIENDESHA HAPA NCHINI.
TAREHE 13-12-2017
Rais wa Jamuhuri ya
Muungano wa Tanzania Mh John Magufuli ameitaka benki kuu ya Tanzania kuzifuta
benki zote ambazo zimeshindwa kujiendesha katika sekta ya kifedha hapa nchini.
Mh Magufuli
ameyasema hayo leo muda mfupi kabla ya kuzindua tawi jipya la benki ya CRDB lililopo
katika jengo la LAPF mjini
Dodoma,ambapo amesema kuwa benki nyingi zimekuwa
hazifanyi vizuri katika sekta ya kifedha hivyo ni lazima benki kuu ianze
kuzichukulia hatua ikiwemo kuzifungia kuliko kuzifumbia macho.
Aidha katika hatua
nyingine rais Magufuli ameitaka benki kuu kudhibiti uingizwaji na matumizi
holela wa fedha za kigeni hapa nchini kuanzia serikalini hadi kwa watu binafsi
kwa kuwa matumizi ya fedha hizo zinaharibu uchumi wa ndani.
Pia Mh Magufuli
amesema kuwa serikali itaendelea kushirikiana na mabenki mbalimbali hapa nchini
ili kuhakikisha sekta hiyo inaendelea kukua kiuchumi na kuwawezesha wananchi
wengi zaidi kukopa katika benki hizo kwa riba nafuu ili waweze kujikwamua na
umaskini.
Hata hivyo katika sherehe hizo rais pia alimkabidhi mkuu wa mkoa
wa Dodoma Dr Bilinith Mahenge kiasi cha shilingi milioni mia moja kwa ajili ya
ujenzi wa wodi ya wagonjwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa huo.
RAIS WA TANZANIA MH. JOHN MAGUFULI AMEITAKA BENKI KUU KUZIFUTA BENKI ZILIZOSHINDWA KUJIENDESHA HAPA NCHINI.
Reviewed by safina radio
on
December 13, 2017
Rating:

No comments