WAZIRI WA NISHATI MH. MERNAD KALEMAN AMETOA SIKU 3 KWA MENEJA WA KUZALISHA UMEME KITUO CHA MTWARA KUREKEBISHA MIUNDO MBINU YA UMEME.
TAREHE 14-12-2017
Waziri wa nishati na madini Mh Mernad Kalemani
ametoa muda wa siku tatu kwa meneja wa umeme kanda ya kusini pamoja na meneja
wa kuzalisha umeme kituo cha Mtwara kurekebisha miundombinu ya umeme inayoenda maeneo
ya wilaya za mkoa wa Lindi na mkoa wa Mtwara.
Mh Kalemani ametoa maagizo hayo wakati wa ziara yake
ya kukagua miradi mbalimbali ya umeme mkoani Mtwara ambapo amesma kuwa ni
lazima wahusika kurekebisha miundombinu hiyo na kujiridhisha kama inafanya kazi
ili wananchi wapate huduma hiyo ya umeme.
Amesema kuwa katika mkoa wa Mtwara kuna umeme wa
kutosha lakini baadhi ya maeneo hayapati umeme na hiyo inatokana na baadhi ya
miundombinu mibovu inayoendelea kukarabatiwa ili kuhakikisha umeme wa kutosha unakuwepo
katika maeneo hayo.
Hata hivyo katika ziara hiyo waziri Kalemani
ametembelea mitambo ya kuzalisha gesi asilia kutoka baharini kuja nchi kavu katika
kituo cha mnazi bey kijiji cha Msimbati kwa ajili ya kuona kiwango cha gesi
kilichopo kama kinatosheleza.
WAZIRI WA NISHATI MH. MERNAD KALEMAN AMETOA SIKU 3 KWA MENEJA WA KUZALISHA UMEME KITUO CHA MTWARA KUREKEBISHA MIUNDO MBINU YA UMEME.
Reviewed by safina radio
on
December 14, 2017
Rating:

No comments