IMEBAINIKA KUWA AJALI NYINGI ZA BARABARANI MKOANI MBEYA ZINASABABISHWA NA MADEREVA KUSHINDWA KUFUATA SHERIA ZA BARABARANI.
TAREHE 06-12-2017
Imeelezwa kuwa ajali nyingi za barabarani zinazotokea mkoani Mbeya kwa kiasi kikubwa zinasababishwa na madereva ambao hawafuati sheria za usalama wa barabarani.
Imeelezwa kuwa ajali nyingi za barabarani zinazotokea mkoani Mbeya kwa kiasi kikubwa zinasababishwa na madereva ambao hawafuati sheria za usalama wa barabarani.
Hayo yameelezwa na kamanda wa kikosi cha usalama wa barabarani mkoa wa Mbeya Bw Leopad
Fungu wakati akizungumza katika mkutano
uliowahusisha madereva wa bodaboda na pikipiki uliofanyika mkoani humo ambapo
amesema kuwa ajali hizo zimekuwa zikipoteza maisha ya watu hasa vijana ambao ni
nguvu kazi ya taifa.
Amesema kuwa kwa mwaka 2016 jumla ya ajali mia nne
na moja za Bajaji ziliripotiwa ambazo
zilisababisha vifo vya watu sabini,ambapo mkoa wa Mbeya ndio unaoongoza kwa
ajali nyingi kati ya mikoa yote hapa nchini hivyo kuna haja ya kila mkazi wa
mkoa huo kufuata sheria za usalama wa barabarani ili kupunguza ajali hizo.
Kwa upande wake afisa mfawidhi wa mamlaka ya nchi
kavu na majini SUMATRA mkoa wa Mbeya Bw Denis Daudi amewataka waendesha Bodaboda
na Bajaji kuzingatia alama za usalama wa barabarani sambamba na kudhibiti
mwendo kasi ili kuhakikisha kuwa suala la ajali linakuwa historia katika mkoa
wa Mbeya.
Kwa upande wa madereva waliohudhuria katika mkutano
huo wamelishukuru jeshi la polisi kupitia kikosi cha usalama barabarani kwa elimu
wanayoendelea kuitoa na nakuahidi kushirikiana na jeshi hilo ili kukomesha
ajali za mara kwa mara mkoani humo.
IMEBAINIKA KUWA AJALI NYINGI ZA BARABARANI MKOANI MBEYA ZINASABABISHWA NA MADEREVA KUSHINDWA KUFUATA SHERIA ZA BARABARANI.
Reviewed by safina radio
on
December 06, 2017
Rating:
No comments