MOURINHO ARUSHIWA MAJI BAADA YA KUCHAPWA MABAO 2-1 NA MANCHESTER CITY

TAREHE 11-12-2017
Manchester City players celebrate after their Derby win at Manchester UnitedHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image cap
Kocha  wa Manchester United Jose Mourinho amerushiwa maji na maziwa kufuatia kushindwa na Manchester City huko Old Trafford.
United walikasirika kutokana na kile walichokiona kuwa kusherehekea kupindukia kwa City kufuatia ushindi wa Jumapili wa bao 2-1  ushindi ambao umefungua  mwanya wa pointi 11 kileleni.
Wachezaji wa City walisherehekea na mashabiki wao baada ya kipenga cha mwisho na maafisa wengine wakajaribu kumshawishi meneja Pep Guardiola kujiunga nao lakini akakataa.
Baada ya wachazaji kuondoka uwanjani inaeleweka kuwa Mourinho alilalamika akiwa ndani ya chumba cha kubadilishia nguo kabla ya kurudi kwa mahojiano.
Upande wa City ulijibu huku kipa wa Brazil Ederson akijibizana na Mourinho kwa lugha ya kireno.
MOURINHO ARUSHIWA MAJI BAADA YA KUCHAPWA MABAO 2-1 NA MANCHESTER CITY MOURINHO ARUSHIWA MAJI BAADA YA KUCHAPWA MABAO 2-1 NA MANCHESTER CITY Reviewed by safina radio on December 11, 2017 Rating: 5

No comments