WAFANYABIASHARA WA MADINI YA TANZANITE WATAKIWA KUTOKUNUNUA MADINI YASIYO NA CHETI.


Naibu waziri wa Madini Mh.Stanslaus  Nyongo amewataka wafanya biashara wa Madini ya Tanzanite nchini kutonunua Madini yasiyokuwa na cheti  cha uhalisia ili kukomesha uuzwaji wa Tanzanite bandia nchini.

Mh. Nyongo ametoa rai hiyo katika mnada wa Madini ya Tanzanite uliofanyika  siku tatu katika mji mdogo wa mererani ikiwa ni Mara ya kwanza kwa mnada huo kufanyika katika mji huo tangu kuanzishwa shughuli za uchimbaji  wa Tanzanite, huku washiriki wakuu katika  Mnada huo wakiwa ni Kampuni ya Tanzanite one na Stamico ambapo kampuni mbili zilijitioa kabla ya mnada kuanza kutokana na kushindwa  masharti.

Aidha amesema serikali ilianzisha hatua ya utoaji vyeti vya uhalisia(certificate of origin)  kwa Madini ya Tanzanite lengo likiwa ni kuzuia uuzwaji wa Madini bandia pamoja na utoroshwaji wa Madini hayo ambapo amewataka wafanya biashara hao kutokununua Madini yasiyoambatana na cheti  cha uhalisia.

Amepongeza hatua  ya rais kuagiza minada  yote ya Madini ya Tanzanite kufanyika katika eneo linalochimbwa Madini hayo ambapo kwa miaka yote minada  imekuwa ikifanyika nje ya eneo hilo jambo ambalo halikuwanufaisha  wazawa wa eneo hilo.

Kwa upande wake  Kamishna wa Madini nchini Benjamini  Mchuampaka amesema kupitia mnada huo serikali imepata zaidi ya shilingi milioni mia moja  huku Halmashauri ya wilaya ya Simanjiro ikitarajia kulipwa zaidi ya shilingi milioni mia tano kama kodi ya huduma  ambapo amesema jumla kuu kutokana na mnada huo ni kiasi cha bilioni  3.

Naye mkuu wa mkoa wa manyara bwana Alexander Mnyeti amewataka wamiliki wa migodi kuhakikisha wanalipa kodi stahiki kwa serikali ambapo amesema serikali imekusudia kuwafutia leseni wale wote ambao hawalipi  kodi huku wakiwa wanaendelea na shughuli za uchimbaji.
WAFANYABIASHARA WA MADINI YA TANZANITE WATAKIWA KUTOKUNUNUA MADINI YASIYO NA CHETI. WAFANYABIASHARA WA MADINI YA TANZANITE WATAKIWA  KUTOKUNUNUA MADINI YASIYO NA CHETI. Reviewed by safina radio on December 22, 2017 Rating: 5

No comments