POLISI 18 WAFARIKI KATIKA SHAMBULIO NCHINI SOMALIA.

Mtu mmoja amejitoa muhanga katika chuo kimoja cha mafunzo ya kipolisi nchini Somalia na kuwaua maafisa wa polisi 18.

Maafisa nchini humo wanasema polisi hao waliokuwa katika mafunzo walikuwa wamekusanyika kwa ajili ya gwaride la asubuhi katika mazingira ya chuo hicho kilichopo mjini Mogadishu wakati shambulizi hilo lilipofanyika.

Watu wengine 15 wamejeruhiwa katika shambulizi hilo linaloshukiwa kufanywa na wanamgambo wa kundi la Al Shabaab.


Hata hivyo Maafisa wanasema idadi ya vifo ingeweza kuwa kubwa zaidi iwapo mshambuliaji huyo angejitoa muhanga katikati ya mkusanyiko mkubwa wa watu.
POLISI 18 WAFARIKI KATIKA SHAMBULIO NCHINI SOMALIA. POLISI 18 WAFARIKI KATIKA SHAMBULIO NCHINI SOMALIA. Reviewed by safina radio on December 15, 2017 Rating: 5

No comments