TANZANIA YASHAURIWA KUUNGA MKONO MASOMO YA UJASIRIAMALI.

Tanzania imeshauriwa kuuunga mkono masomo ya ujasiriamali yanayotolewa na taasisi mbalinbali kwani uwepo wa masomo au kozi hizo utachangia maendeleo hasa kwenye sekta ya viwanda.

Hayo yamelezwa na profesa Emanuel Matiko ambae ni mkuu wa  chuo kikuu cha Arusha wakati akiongea kwenye maafali ya 11 ya chuo hicho.

Profesa Matiko amesema kuwa masomo pekee ya ujasirimali yanaweza kuokoa nchi ya Tanzania kutoka uchumi wa sasa hadi kufikia uchumi wa juu hasa kama yataungwa mkono na serikali

Amefafanua zaidi  kuwa baadhi ya wanafunzi wanaosoma masomo hayo wamekuwa na dhana ya kutaka kujiajiri wenyewe lakini wanashindwa na kuongeza  ikiwa serikali itawasaidia basi dhana ya uchumi wa viwanda ingefika sehemu ambayo imekusudiwa.

Awali  mgeni rasmi katika maafali hayo,ambae ni askofu mkuu jimbo kuu  la kaskazini  mwa Tanzania kanisa la wadventista askofu Godwin Lekundayo amesema kuwa vijana wanapaswa kujiajiri wenyewe na waondokane na dhana kwamba wanapaswa kuajiriwa na serikali.

Askofu Lekundayao amesema kuwa kwa sasa ni ngumu serikali kuweza kuajiri vijana wote wanaomaliza vyuo lakini endapo watatumia elimu ya ujasiriamali watakayoipata kutoka vyuoni itawasidia kujiajiri kwani watatumia elimu hiyo kuzalisha bidhaa na kuweza kufikia uchumi wa kati na hata kuanzisha viwanda.
TANZANIA YASHAURIWA KUUNGA MKONO MASOMO YA UJASIRIAMALI. TANZANIA YASHAURIWA KUUNGA MKONO MASOMO YA UJASIRIAMALI. Reviewed by safina radio on December 18, 2017 Rating: 5

No comments