RAMAPHOSA ATEULIWA KUWA MWENYEKITI MPYA WA ANC.

TAREHE 19-12-2017

Cyril Ramaphosa amechaguliwa kuwa kiongozi mpya wa chama tawala cha ANC nchini A-Kusini .


Makamu wa rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amechaguliwa  kuwa kiongozi wa chama tawala cha African National Congress, ANC, baada ya kushinda kinyang'anyiro kikali ambacho kimedhihirisha mipasuko mikubwa ndani ya chama hicho ambacho kiliongoza vita dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi.

Maelfu ya wafuasi wa Ramaphosa waliimba na kupiga kelele kwenye jumba la mkutano wakati wafuasi wa mgombea aliyeshindwa, Nkosazana Dlamini-Zuma wakionekana kukata tamaa.

Ushindi huo unamuweka Ramaphosa katika nafasi ya kumrithi Rais Jacob Zuma, ambaye utawala wake umekumbwa na kashfa za rushwa, kudorora uchumi na ongezeko la hasira ndani ya chama hicho.

Wajumbe waliosafiri kutoka maeneo mbalimbali ya Afrika Kusini walipiga kura yao baada ya kucheleweshwa mara kadhaa kwa sababu ya kuibuka tofauti kuhusiana na nani alikuwa na haki ya kupiga kura.


Hata hivyo Rais Zuma alijiuzulu kuwa kiongozi wa chama katika mkutano huo, lakini huenda akabakia kuwa kiongozi wa taifa hadi uchaguzi wa mwaka wa 2019.
RAMAPHOSA ATEULIWA KUWA MWENYEKITI MPYA WA ANC. RAMAPHOSA ATEULIWA KUWA MWENYEKITI MPYA WA ANC. Reviewed by safina radio on December 19, 2017 Rating: 5

No comments