NAIBU WA WAZIRI WA ELIMU MH. WILLIUM OLE NASHA AMESEMA SERIKALI ITAENDELEA KUWEKEZA KATIKA ELIMU.

TAREHE 01-12-2017


Naibu Waziri wa Elimu Mh. Willium Ole Nasha amesema kuwa serikali imeendelea kuwekeza katika elimu kwa kutoa kiasi cha shilingi bilioni 427.54 kama mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu.

Akizungumza katika mahafali ya kwanza ya Chuo Kikuu cha Mt. Agustino Tanzania Tawi la Arusha, Mh.Nasha amesema kati ya fedha hizo zilizotolewa na serikali jumla ya shilingi bilioni 100.7 tayari zimeshakwisha kutolewa kama mkopo kwa wanafunzi zaidi ya laki moja kwa mwaka wa kwanza.

Aidha, amewataka maafisa mikopo kutimiza wajibu wao kwa kutoa mikopo kwa wakati ili kuwawezesha wanafunzi kuhudhuria masomo yao vizuri na hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao kwa maafisa ambao hawatatoa mikopo hiyo kwa wakati.

Pia, amewataka wanafunzi wanaotarajia kujiunga na vyuo hapa nchini kuwa makini na kufuata miongozo inayotolewa ikiwa ni pamoja na kuzingatia muda na wakati wa kufanya usahili.


Vile vile, amesema kuwa mmomonyoko wa maadili umekuwa ni janga kubwa katika nchi kutokana na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii hivyo amewataka wahitimu hao kutumia elimu waliyoipata kujiendeleza na kukuza uchumi wa taifa.
NAIBU WA WAZIRI WA ELIMU MH. WILLIUM OLE NASHA AMESEMA SERIKALI ITAENDELEA KUWEKEZA KATIKA ELIMU. NAIBU  WA  WAZIRI  WA  ELIMU  MH. WILLIUM OLE NASHA  AMESEMA SERIKALI   ITAENDELEA KUWEKEZA KATIKA  ELIMU. Reviewed by safina radio on December 01, 2017 Rating: 5

No comments