WAZIRI WA AFYA MH. UMMY MWALIMU AMETOA ONYO KWA WATUMISHI WA AFYA WANAOTOZA GHARAMA ZA MATIBABU WANANCHI WENYE KADI ZA BIMA YA CHF.
TAREHE 07-12-2017
Waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Mh Ummy
Mwalimu ametoa onyo kwa watumishi wa afya hapa nchini wanaotoza gharama za
matibabu wananchi ambao wana kadi za bima ya afya ya jamii CHF.
Mh Ummy ametoa onyo hilo wakati akizungumza na wananchi wa
kijiji cha Humekwa wilayani Chamwino mkoani Dodoma wakati wa kampeni ya usafi
wa mzingira na afya,ambapo amesema kuwa mwananchi mwenye kadi ya CHF anatakiwa
kupata matibabu bure bila usumbufu.
Amesema kuwa kuanzia sasa mtumishi yeyote wa afya atakaye mtoza
mwananchi mwenye kadi ya CHF fedha atachukuliwa hatua kali za kisheria na
amewataka wananchi wote wenye kadi ya bima ya afya kutoa taarifa pale
watakapodaiwa fedha kwa ajili ya kupata huduma za matibabu ili wahusika waweze
kushughulikiwa.
Ameongeza kuwa mikakati ya serikali ni kuhakikisha wananchi wote
wa Tanzania wanapata huduma bora za matibabu na ndio maana bajeti ya wizara
imeongezeka hadi kufikia kiasi cha shilingi bilioni mia mbili,hivyo ni vyema
watumishi wote wa afya wakafuata sheria katika kazi zao za kuwahudumia
wananchi.
Hata hivyo kampeni ya kitaifa ya afya na usafi wa mazingira ya nipo tayari awamu ya
pili inazinduliwa leo na makamu wa rais
wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh Samia Suluhu Hassan.
WAZIRI WA AFYA MH. UMMY MWALIMU AMETOA ONYO KWA WATUMISHI WA AFYA WANAOTOZA GHARAMA ZA MATIBABU WANANCHI WENYE KADI ZA BIMA YA CHF.
Reviewed by safina radio
on
December 07, 2017
Rating:

No comments