VIJANA NCHINI TANZANIA WASHAURIWA KUTUMIA FURSA WALIZONAZO

Vijana wameshauriwa kutumia furusa walizonazo ili kujikwamua kiuchumi ikiwa ni pamoja na kutambua kuwa kiongozi, si kuongoza taasisi au kikundi fulani cha watu pekee bali hata kujiongoza mwenyewe ni uongozi.

Ushauri huo umetolewa na mkurugenzi wa taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya LEAD Tanzania inayotoa mafunzo ya uongozi na jinsi ya kujikwamua kiuchumi kwa vijana Bw.Nickson Kataze katika kongamano la uongozi ambalo limefanyika katika kanisa la K.K.K.T Kimandolu mkoani Arusha.

Bw.Kataze amesema kuwa kijana anapaswa kutumia fursa aliyonayo kujikwamua kiuchumi sambamba na kutambua kuwa yeye ni kiongozi wa maisha yake ambapo taasisi ya LEAD Tanzania imejikita katika kuwawezesha vijana katika maeneo ya elimu, mafunzo ya uongozi,na kuwawezesha kiuchumi.

Aidha ameongeza kuwa shirika hilo tofauti na mashirika mengine walianza kwa kufanya utafiti juu ya changamoto mbalimbali zinazowakabili vijana ambapo walienda katika kata 5 na kuwahoji zaidi ya vijana elfu moja ambapo ripoti ya utafiti huo tayari imewasilishwa kwa mkuu wa wilaya na watendaji wa kata hizo.

Pia katika kongamano hilo vijana mbalimbali kutoka maeneo tofauti ya mkoa wa Arusha walitoa shuhuda jinsi ambavyo mafunzo waliyoyapata katika taasisi hiyo yalivyowasaidia kujikwamua kiuchumi kwa kuweza kuanzisha vitega uchumi ambavyo awali kabla ya kupata mafunzo hayo walikuwa hawana.

Kwa upande wake afisa maendeleo wa jiji la Arusha Bw. Polycap Nguyumba ameitaka taasisi hiyo kuendelea kutoa mafunzo ya uongozi kwa watu mbalimbali yatakayo wasaidia kutoka sehemu moja hadi nyingine na kuongeza kuwa maadili ni msingi wa uongozi.

Hata hivyo taasisi hiyo ya LEAD Tanzania  yenye makao yake katika kanisa la K.K.K.T kimandolu ilianza kazi rasmi mwezi machi mwaka jana ambapo kufikia sasa imefanikiwa kutoa mafunzo ya uongozi kwa zaidi ya watu mia tano na inatarajia kuendelea kutoa mafunzo zaidi na hutolewa bure kwa yeyote anayeitaji.


VIJANA NCHINI TANZANIA WASHAURIWA KUTUMIA FURSA WALIZONAZO VIJANA NCHINI TANZANIA WASHAURIWA KUTUMIA FURSA WALIZONAZO Reviewed by safina radio on December 11, 2017 Rating: 5

No comments