MAANDANO YAZIDI HUKO MASHARIKI YA KATI.

TAREHE 12-12-2017


Eneo la mashariki ya kati limeshuhudia siku ya tano ya maandamano leo kuhusiana na tangazo la rais Donald Trump kuutambua mji wa Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel, wakati shutuma nyingine zaidi zimetolewa kufuatia hatua hiyo yenye utata.

Wakati mamia kwa maelfu ya waandamanaji wakijikusanya nchini Lebanon , waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amekutana na mawaziri wa mambo ya kigeni wa Umoja wa Ulaya mjini Brussels, akisema kwamba hatua hiyo inaleta uwezekano wa kupata amani.

Pia amesema anatarajia wote ama mataifa mengi ya Umoja wa Ulaya yatafuata mfano wa Marekani , lakini mkuu wa sera za mambo ya kigeni wa Umoja huo Federica Mogherini amempinga kwa kusema matarajio yake anaelekeza kwingine.


Mjini Cairo, rais Vladimir Putin wa Urusi  ameshutumu uamuzi wa Trump na kusema unavuruga na kutoa wito wa kuanza tena kwa mazungumzo yaliyokwama kwa muda mrefu.
MAANDANO YAZIDI HUKO MASHARIKI YA KATI. MAANDANO YAZIDI HUKO MASHARIKI YA KATI. Reviewed by safina radio on December 12, 2017 Rating: 5

No comments