RAIS WA UFARANSA EMMANUEL MACRON AMEMTAKA WAZIRI MKUU WA ISRAEL BENJAMIN NETANYAHU ATOE ISHARA YA KUTATUA MGOGORO NA WAPALESTINA .
TAREE 11-12-2017
Netanyahu ameyasema hayo mjini Paris ambapo leo anatarajiwa kukutana na mawaziri wa mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya mjini Brussels, nchini Ubelgiji
Rais wa Ufaransa,
Emmanuel Macron amemtaka Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu awe na
ujasiri na atoe ishara kwa Wapalestina kwa lengo la kutatua mgogoro wa pande
hizo mbili.
Katika mkutano wa
viongozi hao na waandishi wa habari, Macron aliukosoa uamuzi wa rais wa
Marekani ,Donald Trump wa kuitambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel na kutoa
mwito wa kuwepo kwa utulivu.
Macron amesema
Ufaransa inataka suluhisho la nchi mbili zitakazoishi kwa amani ndani ya mipaka
itakayotambuliwa kimataifa.
Kwa upande wake
Netanyahu amesema Jerusalem haijawahi kuwa mji mkuu wa watu wengine wowote na
kwamba Wapalestina watakapoutambua haraka ukweli huu ndipo pande hizo mbili
zitakaposonga mbele katika kuleta amani.
Netanyahu ameyasema hayo mjini Paris ambapo leo anatarajiwa kukutana na mawaziri wa mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya mjini Brussels, nchini Ubelgiji
RAIS WA UFARANSA EMMANUEL MACRON AMEMTAKA WAZIRI MKUU WA ISRAEL BENJAMIN NETANYAHU ATOE ISHARA YA KUTATUA MGOGORO NA WAPALESTINA .
Reviewed by safina radio
on
December 11, 2017
Rating:

No comments