MAREKANI KUUTAMBUA JERUSALEM KAMA MJI MKUU WA ISRAEL

TAREHE 06-12-2017


Maafisa wa serikali ya Marekani wamesema kuwa rais Donald Trump, leo atautambua mji wa Jerusalem kama mji mkuu wa Israel.

Ikulu ya White House imethibitisha kuwa rais Donald Trump pia atazungumza kuhusu juu ya kutangaza rasmi kuhamishia kwa ubalozi wa Marekani Jerusalem.

Kwa mujibu wa msemaji wa ikulu ya white house sarah sanders amesema kuwa Trump alizungumza na baadhi ya viongozi siku ya jumanne kuhusu mipango yake ya kuhamishia ubalozi huo kutoka Tel Aviv kuupeleka Jerusalem.


Wakati huo huo viongozi wa Palestina, Misri, Jordan na Saudi Arabia, wametoa onyo kwa rais Trump kuwa kuhamishia ubalozi huo Jerusalem kutadhoofisha kabisa juhudi za kuleta amani mashariki ya kati. 
MAREKANI KUUTAMBUA JERUSALEM KAMA MJI MKUU WA ISRAEL MAREKANI  KUUTAMBUA  JERUSALEM  KAMA MJI MKUU WA ISRAEL Reviewed by safina radio on December 06, 2017 Rating: 5

No comments