MAKAMU WA RAIS MH. SAMIA SULUHU HASSAN AMETAKA JITIADA MBALIMBALI ZIFANYIKE KUPUNGUZA MAAMBUKIZI YA UKIMWI
TAREHE 01-12-2017
Makamu wa rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania
Mh Samia Suluhu Hassan ametaka jitihada mbalimbali kufanyika ili kupunguza
maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa vijana hapa nchini.
Mh Suluhu ameyasema hayo leo wakati akiwa mgeni
rasmi katika maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani iliyofanyika kitaifa jijini
Dar-es-salaam,ambapo amesema kuwa endapo juhudi za ziada zitafanywa kati ya
serikali,taasisi binafsi pamoja na wananchi kupambana na ugonjwa huo idadi ya
vijana wanaoathirika na ukimwi itapungua kwa kiasi kikubwa.
Amesema kuwa,inasikitisha kuona idadi ya waathirika
wengi wa maambukizi ya virusi vya ukimwi ni wasichana wadogo,ambapo pia
ametumia maadhimisho hayo kuwaonya wababa na wazee wanaowarubuni wasichana hao
ili washiriki nao vitendo vya ngono kuacha tabia hiyo mara moja kwani
watakapobainika hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.
Kwa upande wake mkurugenzi wa kudhibiti maambukizi
ya virusi vya ukimwi hapa nchini TACAIDS Dr Leonad Maboko amesema kuwa licha ya
maambukizi hayo kupungua hapa nchini bado kuna changamoto kwa vijana katika
kukabiliana na ugonjwa huo.
Katika maadhimisho hayo pia makamu wa rais alizindua
taarifa ya maambukizi wa virusi vya ukimwi,ambapo mikoa ya Njombe na Iringa
ndio inayoongoza kwa asilimia kubwa ya watu waloathirika na ugonjwa huo.
Hata hivyo maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani
huadhimishwa kila ifikapo Desemba Mosi ya kila mwaka,ambapo kauli mbiu ya mwaka
huu ni Changia Mfuko wa Udhamini wa Ukimwi Okoa Maisha.
MAKAMU WA RAIS MH. SAMIA SULUHU HASSAN AMETAKA JITIADA MBALIMBALI ZIFANYIKE KUPUNGUZA MAAMBUKIZI YA UKIMWI
Reviewed by safina radio
on
December 01, 2017
Rating:

No comments