RAIS WA TANZANIA MH. JOHN MAGUFULI AMEKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA RAIS WA KAMPUNI YA TOTAL MUMAN NGUWERE

TAREHE 05-12-2017


Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh John Pombe Magufuli leo amekutana na kufanya mazungumzo na rais wa kampuni ya TOTAL Muman Nguwere ikulu jijini Dar-es-salaam.

Katika mazungumzo hayo rais Magufuli na mgeni wake wamejadili masuala mbalimbali kuhusu kazi za kampuni ya Total na utafiti wa mafuta unaofanywa na kampuni hiyo katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Wakizungumza mara baada ya mazungumzo hayo waziri wa viwanda na biashara Mh Charles Mwijage na waziri wa nishati Mh Mernad Kaleman wamesema kuwa mikakati ya uwekezaji unaofanywa na kampuni ya Total hapa nchini utasaidia kukuza sekta ya viwanda hapa nchini pamoja na sekta ya nishati.

Katika hatua nyingine rais John Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na balozi wa umoja wa Falme za Kiarabu Abdulah Ibrahim Al Swaid na ujumbe wake.

Katika mazungumzo hayo viongozi hao wamezungumza masuala mbalimbali ya ushirikiano
RAIS WA TANZANIA MH. JOHN MAGUFULI AMEKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA RAIS WA KAMPUNI YA TOTAL MUMAN NGUWERE RAIS WA TANZANIA MH. JOHN MAGUFULI AMEKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA RAIS WA KAMPUNI YA TOTAL MUMAN NGUWERE Reviewed by safina radio on December 05, 2017 Rating: 5

No comments