SERIKALI IMEWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUACHA KUFANYA KAZI KWA MAZOEA.

Serikali imewataka watumishi wote wa uma hapa nchini kuacha kufanya kazi kwa mazoea na badala yake wafanye kazi kwa ufanisi  ili waweze kufikia hazima ya serikali ya awamu ya tano ya kukuza  uchumi wake kwa njia ya viwanda.

Hayo yamesemwa leo  na naibu waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Dr.Faustine Ndugulile,wakati akizungumza na wafanyakazi wa taasisi ya maendeleo ya jamii Tengeru mkoani 

Arusha,ambapo amesema kuwa ili hazma ya kukuza uchumi wa nchi kwa njia ya viwanda ifanikiwe ni lazima kila mfanyakazi afanye kazi kwa bidii.
Aidha Dr Ndugulile amesema kuwa taasisi ya maendeleo ya jamii Tengeru ndio chachu ya wataalamu ambao majukumu yao ni kuhakikisha  kwamba wanaisaidia serikali kuamsha hari ya wananchi kwa kushiriki kwao katika shughuli mbalimbali za maendeleo.


Kwa upande wake mkurugenzi wa taasisi ya maendeleo ya jamii Tengeru Dr,Patrick Golwite ameahidi kufanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa na naibu waziri  ikiwa ni pamoja na kulipatia ufumbuzi tatizo la mpaka kati ya chuo cha mifugo na taasisi ya maendeleo ya jamii Tengeru.   
SERIKALI IMEWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUACHA KUFANYA KAZI KWA MAZOEA. SERIKALI IMEWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUACHA KUFANYA KAZI KWA MAZOEA. Reviewed by safina radio on December 15, 2017 Rating: 5

No comments