UJERUMANI YALAANI KITENDO CHA KUCHOMWA MOTO BENDERA YA ISRAEL

TAREHE 12-12-2017


Serikali ya Ujerumani imelaani kitendo cha kuichoma moto bendera ya Israel kilichofanywa na watu walioshiriki katika maandamano ya kuwaunga mkono Wapalestina mjini Berlin na kupinga uamuzi wa Rais wa Marekani, Donald Trump wa kuutambua Jerusalem kuwa ni mji mkuu wa Israel.

 Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel amesema serikali yake inapinga aina zote za chuki dhidi ya Wayahudi na wageni.

Kansela Merkel ameeleza kwamba hakuna tofauti zozote za mitazamo zinazoweza kuhalalisha vitendo kama hivyo hata ikiwa ni kuhusu suala la mji wa Jerusalem.

Waziri wa Mambo ya Ndani Thomas de Maizière na wa Mambo ya Nje, Sigmar Gabriel wametamka kuwa vitendo kama hivyo haviwezi kuvumiliwa.

Hata ivyo Baraza kuu la Wayahudi nchini Ujerumani limeelezea wasiwasi wake juu ya matukio ya kuchomwa moto bendera ya Israel.



UJERUMANI YALAANI KITENDO CHA KUCHOMWA MOTO BENDERA YA ISRAEL UJERUMANI YALAANI KITENDO CHA KUCHOMWA MOTO BENDERA YA ISRAEL Reviewed by safina radio on December 12, 2017 Rating: 5

No comments