WATANZANIA WASHAURIWA KUTUMIA SEHEMU YA MAPATO YAO KUSAIDIA YATIMA NA WASIOJIWEZA.
TAREHE 27-12-2017
Watanzania wametakiwa kujijengea tabia ya kutumia
sehemu ya mapato yao kwa ajili ya kuwasaidia watoto yatima na watu wasiojiweza
katika jamii ili kuwawezesha kujikwamua na umasikini na kufikia ndoto zao.
Hayo yamesemwa na operation meneja wa kampuni inayojihusisha na utalii wa kitamaduni ya Tengeru
cultural tourism Bw. Ruben Samweli Palangyo wakati akikabidhi msaada wa vyakula
na vinywaji kwa watoto yatima katika vituo vya yatima vya Global na Ikunda
vilivyopo wilayani Arumeru mkoani Arusha.
Bw. Pallangyo amesema kuwa kampuni hiyo imejiwekea
utaratibu wa kutumia sehemu ya mapato yake kusaidia yatima na watu wasiojiweza
katika jamii kwani hawajapenda kuishi maisha waliyonayo hivyo ni vyema
makampuni mengine na watu binafsi kutenga sehemu ya mapato yao kuwasaidia.
Kwa upande wake mratibu wa Tengeru cultural tourism
Bi. Sara Gadi amesema kuwa wameguswa na uhitaji wa watoto yatima ndio maana
wamejiwekea utaratibu wa kutumia sehemu ya pato lao kuwasaidia na kuitaka jamii
kuungana kwa pamoja kuwasaidia yatima na watu wasiojiweza katika jamii.
Bi. Sara ameongeza kuwa ni vyema jamii nzima ikaungana kwa pamoja kuwasaidia yatima kwani hawakupenda kupoteza wazazi wao na bado wana ndoto kubwa katika maisha yao kama walivyo watoto wenye wazazi na wakuwasaidia ni jamii.
Naye mlezi wa kituo cha Ikunda Mchungaji Betrice
Izrael Kishe amesema kuwa kazi ya kulea yatima ni wito kutoka kwa Mungu hivyo
wenye vituo hawapaswi kuzunguka kuomba misaada kwani mwenye kituo ni Mungu na
atawatumia watu kupeleka misaada.
Aidha Bw. Macdonald Elifasi Kaaya mlezi wa watoto katika kituo cha Global ameishukuru kampuni ya Tengeru cultural tourism kwa msaada walioutoa na kuwataka watu mbalimbali kutumia njia ya kusaidia yatima kuteka baraka lakini pia kama njia ya kumtumikia Mungu.
Hata hivyo Zakaria Simon kutoka kituo cha global orphanage
kwa niaba ya wenzake ameishukuru kampuni hiyo kwa kuwambuka.
WATANZANIA WASHAURIWA KUTUMIA SEHEMU YA MAPATO YAO KUSAIDIA YATIMA NA WASIOJIWEZA.
Reviewed by safina radio
on
December 27, 2017
Rating:
No comments