MKUU WA MKOA WA TABORA AGREY MWANRY AKABIDHI MAONI KWA MKUU WA POLISI IGUNGA.
TAREHE 20-12-2017
Mkuu wa mkoa wa
Tabora Bw Agrey Mwandry amemkabidhi mkuu wa polisi wa wilaya ya Igunga kura za
maoni zenye majina ya watu wanaojihusisha na vitendo vya uhujumu wa miondombinu
ya umeme wilayani humo.
Bw Mwandry
amekabidhi majina hayo baada ya kuendesha kura ya maoni katika vitongoji vya
Mkongoro na Makomelo katika mji mdogo wa Igunga kutokana na kuibuka kwa vitendo
vya kuhujumu njia kuu za usambazaji umeme ujulikanao kama Back Bone inayopita
katika vitongoji hivyo.
Pia Bw Mwandry
amemwagiza mkuu huyo wa polisi wa wilaya
ya Igunga kwenda kutumia majina hayo kama chanzo cha upelelezi ili kujua ni
nani anayehusika na vitendo hivyo vya uharibifu wa miundombinu ya umeme ambayo
serikali inatumia gharama kubwa kuitekeleza.
Nao wataalamu wa
umeme kutoka shirika la umeme hapa nchini mkoani Tabora na makao makuu
wamewaonya wanachi kuacha kuhujumu miundombinu hiyo kwani kwa kufanya hivyo
wataathiri maisha yao na maendeleo ya nchi kiujumla.
MKUU WA MKOA WA TABORA AGREY MWANRY AKABIDHI MAONI KWA MKUU WA POLISI IGUNGA.
Reviewed by safina radio
on
December 20, 2017
Rating:

No comments