WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS UTUMISHI NA UTAWALA BORA MH. GEORGE MKUCHIKA ATOA MAAGIZO KWA WAKURUGENZI WA HALMASHAURI ZOTE HAPA NCHINI.

TAREHE 12-12-2017


Waziri wa nchi ofisi ya rais utumishi na utawala bora Mh George Mkuchika amewataka wakurugenzi wa halmashauri zote hapa nchini kuwafukuza kazi wafanyakazi wote wa mfuko wa maendeleo ya jamii nchini TASAF walioshiriki kuingiza majina ya watu ambao hawastahili kusaidiwa na mfuko huo.

Mh Mkuchika ameyasema hayo mkoani Tanga wakati akizungumza na viongozi wa mkoa huo wakiwemo watendaji wa TASAF,ambapo amesema kuwa lengo na mpango wa mfuko huo ni kunufaisha kaya maskini hivyo serikali haitawavumilia wale wote wanaoenda kinyume na malengo hayo.

Amesema kuwa pamoja na nia njema ya kuanzishwa kwa mfuko wa TASAF hapa nchini kuna baadhi ya watu wanaoharibu sifa za mfuko huo kwa kusajili watu ambao hawakustahili kusahiliwa kutokana na sheria kukiukwa na rushwa kutamalaki jambo linalosababisha watu wanyonge kukosa haki zao za msingi.


Kwa upande wake katibu tawala wa mkoa wa Tanga Mhandisi Zela Said amesema kuwa hadi sasa kaya elfu hamsini na tano mia saba na arobaini na tatu zimenufaika na mpango huo wa kunusuru kaya maskini mkoani humo.
WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS UTUMISHI NA UTAWALA BORA MH. GEORGE MKUCHIKA ATOA MAAGIZO KWA WAKURUGENZI WA HALMASHAURI ZOTE HAPA NCHINI. WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS UTUMISHI NA UTAWALA BORA MH. GEORGE MKUCHIKA ATOA MAAGIZO KWA  WAKURUGENZI WA HALMASHAURI ZOTE HAPA NCHINI. Reviewed by safina radio on December 12, 2017 Rating: 5

No comments