WAZIRI MKUU WA TANZANIA MAJALIWA KASSIM MAJALIWA AMESEMA SERIKALI IMEWEKA MAZINGIRA MAZURI YA UPATIKANAJI WA VIWANJA KWA AJILI YA UJENZI.

TAREHE 07-12-2017


Waziri mkuu wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh Majaliwa Kassimu Majaliwa amesema kuwa serikali imeweka mazingira mazuri ya kuwezesha upatikanaji wa viwanja kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za mashirika mbalimbali ya Kimatifa mkoani Dodoma.

Mh majaliwa ameyasema hayo mkoani Dodoma wakati wa uzinduzi wa ofisi za umoja wa mataifa,ambapo amesema kuwa uzinduzi wa ofisi hizo ni ishara za kuunga mkono jitihada za serikali za kuhamia Dodoma.

Amesema kuwa mbali na serikali kuweka mazingira mazuri kwa ajili ya kuwezesha ujenzi wa ofisi za mashirika hayo pia itatoa msaada wa huduma za namna ya kuanzisha ujenzi wake hivyo kwa mashirika ambayo yako tayari wawasiliane na meya wa manispaa ya Dodoma ili wapate viwanja hivyo.

Ameongeza kuwa kwa kutambua kuwa Dodoma ni makao makuu ya nchi sherehe zote za kitaifa ikiwemo za uhuru kuanzia sasa zitaanza kufanyika mkoani Dodoma.


Kw upande wake waziri wa mambo ya nje ushirikiano wa Afrika Mashariki kikanda na mataifa Balozi Agustine Mahiga amesema kuwa,wizara yake itasaidia kuwezesha juhudi za serikali kuhamia Dodoma pamoja na kusimamia amani ili kuleta maendeleo kwa watu wake.
WAZIRI MKUU WA TANZANIA MAJALIWA KASSIM MAJALIWA AMESEMA SERIKALI IMEWEKA MAZINGIRA MAZURI YA UPATIKANAJI WA VIWANJA KWA AJILI YA UJENZI. WAZIRI MKUU WA TANZANIA MAJALIWA KASSIM MAJALIWA  AMESEMA SERIKALI IMEWEKA MAZINGIRA MAZURI YA UPATIKANAJI WA  VIWANJA KWA  AJILI  YA  UJENZI. Reviewed by safina radio on December 07, 2017 Rating: 5

No comments