MKUU WA MKOA WA MOROGORO ATOA ONYO KWA WAZAZI WANAOWAACHISHA WATOTO WA KIKE SHULE MKOANI HUMO.

TAREHE 15-12-2017



Mkuu wa mkoa wa Morogoro Dk. Kebwe Steven Kebwe amewakemea vikali hususani wazazi wa jamii ya kimaasai kwa kitendo cha kuwakatisha masomo watoto wa kike na kuwaozesha ambapo amesema hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya watakaokamatwa wakijihusisha na vitendo hivyo.

Dk. Kebwe ametoa agizo hilo akiwa katika viwanja vya shule ya sekondari Parakuyo wilayani Kilosa mkoani Morogoro, wakati akiongoza zoezi la kuchangisha fedha za  ujenzi wa bweni la wasichana wa shule hiyo ambapo asilimia kubwa ya wanafunzi katika shule hiyo wanatoka katika jamii ya wafugaji ya kimasai.

Mkuu huyo wa mkoa amesema kuwa kumekuwa na mchezo mchafu kwa jamii za wafugaji kuwaachisha shule watoto wa kike  na kuwaozesha jambo ambalo halikubaliki katika uongozi wake na kumwagiza mkuu wa Wilaya ya Kilosa kusimamia kwa karibu maagizo hayo.


Aidha amewataka wazee kuacha mara moja tabia ya kuoa watoto wadogo na badala yake kuwaacha waende shule na kuongeza kuwa atakayekiuka maagizo hayo sheria itachukua mkondo wake bila kujali umri wa mhusika.
MKUU WA MKOA WA MOROGORO ATOA ONYO KWA WAZAZI WANAOWAACHISHA WATOTO WA KIKE SHULE MKOANI HUMO. MKUU WA MKOA WA MOROGORO ATOA ONYO KWA WAZAZI WANAOWAACHISHA WATOTO WA KIKE SHULE MKOANI HUMO. Reviewed by safina radio on December 15, 2017 Rating: 5

No comments