WATU WENYE ULEMAVU WAMETAKIWA KUSHIRIKI KIKAMILIFU KATIKA SHUGHULI ZAO NA ZA UJENZI WA TAIFA.
TAREHE 05-12-2017

Shirikisho la watu
wenye ulemavu SHIVIWATA hapa nchini mkoani Rukwa limewataka watu wenye ulemavu
kushiriki kikamilifu katika shughuli zao pamoja na za ujenzi wa taifa.
Wito huo umetolewa
na katibu mkuu wa shirikisho hilo Bi Elina John wakati akizungumza katika
maadhimisho ya watu wenye ulemavu mkoani humo,ambapo amewataka walemavu hao
kuacha kujitenga kushiriki katika shughuli za kijamii kwa madai ya kuwa
walemavu.
Bi Elina amesema
kuwa,endapo walemavu watashiriki kikamilifu katika shughuli mbalimbali za
maendeleo wataweza kujipatia kipato na kujikwamua katika hali ya umaskini ikiwa
ni pamoja na kuondoa dhana ya kwamba mlemavu hawezi kushiriki katika shughuli
za ujenzi wa taifa.
Kwa upande wake
afisa maendeleo ya jamii mkoa wa Rukwa Bw Godfrey Mapunda amesema kuwa kuna
haja ya kufahamu takwimu sahihi za watu wenye ulemavu hapa nchini ili kuwezesha
serikali kupanga bajeti yao.
WATU WENYE ULEMAVU WAMETAKIWA KUSHIRIKI KIKAMILIFU KATIKA SHUGHULI ZAO NA ZA UJENZI WA TAIFA.
Reviewed by safina radio
on
December 05, 2017
Rating:

No comments