WATU 15 WANYONGWA NCHINI MISRI.
Serikali
ya Misri imewanyonga watu 15 waliotiwa hatiani kwa mauaji ya wanajeshi tisa
mwaka 2013 katika jimbo la Sinai kaskazini mwa nchi hiyo.
Mahakama
ya kijeshi iliyokuwa ikisikiliza mashitaka dhidi ya walalamikaji ilitupilia
mbali rufaa yao na kuunga mkono hukumu ya awali.
Watu
hao walitiwa hatiani kwa kuhusika na mauaji ya Sajenti mmoja wa jeshi na
wanajeshi wengine saba katika rasi ya Sinai miaka minne iliyopita.
Misri
imekuwa ikikabiliwa na mashambulizi yanayofanywa na makundi ya itikadi kali
mengi yakivilenga vikosi vya usalama na jamii ya wakristo wachache tangu
mapinduzi yaliyofanywa na jeshi kumuondoa aliyekuwa rais wa nchi hiyo Mohamed
Morsi mwaka 2013.
Novemba
mwaka huu zaidi ya waumini 300 waliuawa katika msikiti mmoja kaskazini mwa
Sinai likiwa ni shambulizi baya zaidi la hivi karibuni katika historia ya nchi
hiyo.
WATU 15 WANYONGWA NCHINI MISRI.
Reviewed by safina radio
on
December 27, 2017
Rating:
No comments