WATANZANIA WASHAURIWA KUJENGA MADHABAHU YA MUNGU ILI KUTEKA MALANGO YA MAFANIKIO.

Zikiwa zimebaki siku chache kumaliza mwaka 2017 Watanzania wameshauriwa kujenga madahabahu ya Mungu katika mwaka mpya 2018 ili kuteka malango ya mafanikio yao na kuishi bila kusumbuliwa na magonjwa,umaskini pamoja na nguvu za giza.

Redio safina kesho katika ukumbi wa maombi ulioko mbauda jijini Arusha kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa sita na nusu mchana itawafundisha watu umuhimu wa kuteka mwaka na kufikia malengo kwa kuujengea madhabahu ya Mungu.

Aidha kulingana na somo hilo imebainika kuwa mafanikio ya mtu kimaisha hutegemea nguvu ya madhabahu iliyomshikilia nafsi yake ambapo mengine humfunga mtu asiweze kufanikiwa kiuchumi na kiroho.

Pia mafundisho hayo yatakwenda sambamba na watu kufundishwa namna ya kujenga madhabahu ya Mungu kwenye shughuli zao za kila siku kama vile kilimo na ufugaji,elimu na biashara,vipawa na karama pamoja na huduma kwa ujumla.


Hata hivyo watu watapaswa kuja na kalenda mpya ya mwaka wa 2018 ambapo maombi rasmi yatafanyika ili watu waweze kuishi kwa amani bila kukumbwa na majanga yoyote baada ya kubomoa madhabahu ya miungu iliyojengwa na shetani ndani ya watu na kazi zao.
WATANZANIA WASHAURIWA KUJENGA MADHABAHU YA MUNGU ILI KUTEKA MALANGO YA MAFANIKIO. WATANZANIA WASHAURIWA KUJENGA MADHABAHU YA MUNGU ILI KUTEKA MALANGO YA MAFANIKIO. Reviewed by safina radio on December 13, 2017 Rating: 5

No comments