WAZIRI JAFFO AMEMPA SIKU 20 MKANDARASI ANAYEJENGA WODI YA KINA MAMA KATIKA ZAHANATI YA MKUNZI.

TAREHE 12-12-2017


Waziri wa nchi ofisi ya rais tawala za mikoa na serikali za mitaa Mh Suleman Jaffo amempa siku 20 mkandarasi anayejenga wodi ya akina mama na watoto katika zahanati ya Mkunzi iliyopo wilayani Muheza mkoani Tanga kukamilisha ujenzi huo.

Mh Jaffo ametoa kauli hiyo wakati wa ziara yake ya siku moja ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo wilayani Muheza,ambapo amesema kuwa serikali inafanya kila liwezekanalo kuboresha huduma za afya,hivyo mkandarasi huyo anatakiwa kukamilisha wodi hiyo ili wananchi wapate huduma bora za matibabu.

Aidha amewataka watendaji wa serikali kutumia vizuri fedha za miradi ya maendeleo zinazotolewa na serikali kwa matumizi yaliyokusudiwa na si vinginevyo.


Hata hivyo waziri huyo amempongeza mkuu wa wilaya ya Muheza pamoja na viongozi wengine kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo ya kuhakikisha huduma za afya zinaendelea kuwa bora hapa nchini.
WAZIRI JAFFO AMEMPA SIKU 20 MKANDARASI ANAYEJENGA WODI YA KINA MAMA KATIKA ZAHANATI YA MKUNZI. WAZIRI JAFFO AMEMPA SIKU 20  MKANDARASI ANAYEJENGA WODI YA KINA MAMA KATIKA ZAHANATI YA MKUNZI. Reviewed by safina radio on December 12, 2017 Rating: 5

No comments