SERIKALI KUENDELEA KUSAIDIA KAYA MASIKINI NCHINI.

TAREHE 05-12-2017
                                                 

Serikali imesema kuwa itaendelea kuzisaidia kaya mbalimbali hapa nchini kuondokana na hali ya umaskini kupitia mfuko wake wa kusaidia kaya maskini wa TASAF.

Hayo yameelezwa na mtendaji mkuu wa mfuko wa kusaidia kaya maskini hapa nchini wa TASAF Bw Ladslaous Mwamanga wakati akielezea mafanikio ya mfuko huo mbele ya waandishi wa habari jijini Dar-es-salaam,ambapo amesema kuwa juhudi kubwa za serikali ni kuendelea kuwezesha kaya zote ambazo ziko kwenye hali ya umaskini uliokithiri ili ziweze kujikimu na kupata mahitaji ya msingi.

Bw Mwamanga amesema kuwa tangu mfuko wa TASAF uanze kazi zake ya kuwahudumia wananchi kaya nyingi hapa nchini zimepiga hatua kutoka katika umaskini uliokithiri kuelekea kwenye maendeleo na mafanikio makubwa.


Amesema mafanikio ya TASAF ni mwendelezo wa kuwapa fursa walengwa wa mfuko huo kushiriki katika sekta za maendeleo endelevu kwa manufaa yao binafsi na kwa taifa kwa ujumla.
SERIKALI KUENDELEA KUSAIDIA KAYA MASIKINI NCHINI. SERIKALI  KUENDELEA KUSAIDIA KAYA MASIKINI NCHINI. Reviewed by safina radio on December 05, 2017 Rating: 5

No comments