WAZIRI TILLERSON ASEMA MAREKANI IKO TAYARI KWA MAZUNGUMZO NA KOREA KASKAZINI.
TAREHE 13-12-2017

Waziri wa
mashauri ya nchi za kigeni wa Marekani Rex Tillerson amesema Marekani iko
tayari kwa mazungumzo wakati wowote na Korea Kaskazini bila ya masharti yoyote.
Taaarifa yake imeonekana
kuwa tofauti na msimamo wa awali wa Marekani kuwa Korea Kaskazini ni lazima
iharibu zana zake kabla ya mazungummzo yoyote kufanyika.
Lakini saa chache
baadaye Ikulu wa White House ilisema msimamo wa Trump kwa Korea Kaskazini haujabadilika, huku
hatua ya Korea Kaskazini ya kuunda zana za nyuklia ikisababisha Marekani kuongeza
vikwazo vikubwa dhidi ya nchi hiyo.
Kando na hilo mkuu wa
masuala ya siasa wa Umoja wa Mataifa ambaye hivi karibu alizuru Korea Kaskazini
aliwaambia waandishi wa habari kuwa maafisa wa Korean Kaskazini wanaamini kuwa
ni muhimu kuzuia vita.
Uhusiano wa
kidiplomasia kati ya Marekani na Korea Kaskazini umeharibika kufuatia majaribio
ya hivi karibuni ya mabomu ya nyuklia na makombora na kuwepo vita vya Maneno
kati ya rais wa Marekani Donald Trump na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim
Jong-un.
Hata hivyo akizungumza
kwenye mkutano wa baraza la nchi za Atlantic siku ya Jumanne, Bw Tillerson
alisema kuwa Marekani haiwezi kukubali Korea Kaskazini kujihami kwa silaha za
nyuklia.
WAZIRI TILLERSON ASEMA MAREKANI IKO TAYARI KWA MAZUNGUMZO NA KOREA KASKAZINI.
Reviewed by safina radio
on
December 13, 2017
Rating:
No comments