RAIS JACOB ZUMA AMEAMRIWA NA MAHAKAMA KUANZISHA UCHUNGUZI WA MADAI YA RUSHWA DHIDI YA SERIKALI.

TAREHE 14-12-2017


Mahakama kuu nchini Afrika Kusini imemuamuru rais Jacob Zuma aanzishe uchunguzi katika kipindi cha siku 30 juu ya madai ya rushwa dhidi ya serikali yake.

Mahakama hiyo imetoa agizo hilo baada ya uchunguzi uliofanyika kufichua uhalifu wa kiwango cha juu na ufisadi kutokana na uhusiano wa rais Zuma na familia ya Gupta wafanyabishara matajiri wakubwa ambao wanatuhumiwa kupata kandarasi nono za serikali na kuwa na ushawishi mkubwa katika maamuzi ya serikali.

Hata hivyo madai hayo yamekanushwa na rais Zuma pamoja na familia ya Gupta.

 Zuma amekuwa anashinikizwa ajiuzulu kutokana na madai hayo.
RAIS JACOB ZUMA AMEAMRIWA NA MAHAKAMA KUANZISHA UCHUNGUZI WA MADAI YA RUSHWA DHIDI YA SERIKALI. RAIS JACOB ZUMA AMEAMRIWA NA MAHAKAMA KUANZISHA UCHUNGUZI WA MADAI YA RUSHWA DHIDI YA SERIKALI. Reviewed by safina radio on December 14, 2017 Rating: 5

No comments