MKUU WA JESHI LA POLISI JENERALI SAIMON SIRRO AMEWATAKA RAIA WAPYA WA BURUNDI KUJIEPUSHA NA VITENDO VYA UHALIFU

TAREHE 11-12-2017



Mkuu wa jeshi la polisi nchini insipekta jenerali Saimon Sirro amewataka raia wapya wa Burundi waliokuwa wakiishi katika kambi za Mishamo na Katumba mkoani Katavi na Ulyankulu mkoani Tabora  kujiepusha na vitendo vya uhalifu.

 IGP Sirro ametoa kauli hiyo kufuatia baadhi ya raia hao wapya kujihusisha na vitendo vya ujambazi wa kutumia silaha, kuingiza silaha kutoka nchini mwao,pamoja na wahamiaji haramu vitendo ambavyo ni kinyume na sheria za Tanzania.

Sirro amewataka raia hao wapya kuwa wazalendo,  raia wema, na washirikiane na watanzania wenzao  kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo na yeyote atakayebainika kijihusisha na uhalifu ajue kwamba vyombo vya ulinzi na usalama vitawafuatilia.

Aidha amewahakikishia wakazi wa mkoa wa Tabora na nchi nzima kuwa jeshi la polisi limejijenga na liko kamilifu kukabiliana na uhalifu wa aina mbalimbali hivyo amewataka wananchi kutekeleza kazi zao bila wasiwasi wowote.

Hata hivyo Sirro yupo mkoani Tabora kukagua kazi mbalimbali na utendaji  kazi wa jeshi la polisi na kuwahimiza askari wa jeshi hilo kuwatumikia wananchi kwa kuzingatia kanuni, taratibu na sheriaza nchi.


MKUU WA JESHI LA POLISI JENERALI SAIMON SIRRO AMEWATAKA RAIA WAPYA WA BURUNDI KUJIEPUSHA NA VITENDO VYA UHALIFU MKUU WA JESHI LA POLISI JENERALI SAIMON SIRRO AMEWATAKA RAIA WAPYA WA  BURUNDI KUJIEPUSHA NA VITENDO VYA UHALIFU Reviewed by safina radio on December 11, 2017 Rating: 5

No comments