RAIS WA ZIMBABWE EMMERSON MNANGAGWA ATEUA BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI
TAREHE 01-12-2017
Rais mpya wa Zimbabwe Emerson Mnangagwa ameteua baraza jipya la mawaziri linalojumuisha wanachama watiifu kwa chama tawala nchini humo pamoja na maafisa wa jeshi la nchi hiyo ambalo hatua yake ilisaidia kumuondoa madarakani aliyekuwa rais wa nchi hiyo Robert Mugabe.
Hata
hivyo hakuna mwanasiasa wa upinzani aliyejumuishwa katika baraza hilo jipya
ambalo linaonekana kuwa jaribio la kwanza kwa Mnangagwa mshirika wa muda mrefu
wa Mugabe, iwapo ataongoza pasipo kivuli cha Mugabe.
Miongoni
mwa wanaounda baraza hilo lenye mawaziri 22 lililotangazwa jana jioni kupitia
televisheni ya taifa nchini humo ni pamoja na Meja Jenerali Sibusiso Moyo
ambaye anakuwa waziri wa mambo ya nje na Chris Mutsvangwa kiongozi wa
maveterani wa kivita aliyeteuliwa kuwa waziri wa habari.
Novemba
15 , Moyo alitangaza jeshi kuchukua mamlaka hatua iliyoenda sambamba na Mugabe
kuwekwa katika kizuizi cha ndani na baadaye kujiuzulu na kuhitimisha utawala
wake uliodumu kwa miaka 37.
RAIS WA ZIMBABWE EMMERSON MNANGAGWA ATEUA BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI
Reviewed by safina radio
on
December 01, 2017
Rating:

No comments