RAIS TRUMP ATANGAZA RASMI KUUTAMBUA JERUSALEM KUWA MJI MKUU WA ISRAEL

TAREHE 07-12-2017




Rais Donald Trump wa Marekani ametangaza rasmi kuitambua Jerusalem kama mji mkuu wa Israel licha ya uamuzi huo kupingwa na viongozi kadhaa wa kidunia.

Kufuatia tangazo hilo la Trump ubalozi wa Marekani sasa utahamishwa kutoka mjini Tel Aviv na kupelekwa Jerusalem.

Akizungumza  katika ikulu ya Marekani White House Trump amesema ni muda muafaka sasa kuitambua rasmi Jerusalem kama mji mkuu wa Israel na kuongeza kuwa hatua hiyo ni ishara ya kutambua ukweli uliopo kuhusiana na suala hilo.

Amesema wakati alipoingia madarakani aliahidi kuangalia kwa makini changamoto zinazoikabili dunia na kuwa hauwezi kutafuta suluhisho la matatizo kwa kutumia njia zilezile zilizoshindwa.

Kufuatia hatua hiyo katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amekosoa hatua hiyo na kusema hakuna mpango mbadala zaidi ya shirikisho la mataifa mawili,ambapo pia baraza la usalama la Umoja wa Mataifa linatarajia kukutana katika kikao cha dharura ikiwa ni baada ya rais Donald Trump kutangaza uamuzi huo.


RAIS TRUMP ATANGAZA RASMI KUUTAMBUA JERUSALEM KUWA MJI MKUU WA ISRAEL RAIS TRUMP ATANGAZA RASMI KUUTAMBUA  JERUSALEM  KUWA MJI  MKUU WA  ISRAEL Reviewed by safina radio on December 07, 2017 Rating: 5

No comments